The House of Favourite Newspapers

Dogo Janja: Bila Mimi Young Killer Atakufa Njaa

0
Dogo Janja.

MWANAMUKIZI anayefanya vizuri kwenye Tasnia ya Bongo Fleva na wimbo wake uitwao Kidebe, Abdulazizi Chende, ‘Dogo Janja’ amefunguka kuwa bila yeye mshindani wake mkubwa katika muziki huo, Erick Msodoki “Young Killer’ hawezi kufika popote maana atakosa kiki na zaidi atakufa njaa.

Akichonga na Uwazi Showbiz, Dogo Janja alisema kuwa amemfuatilia Young Killer katika kazi zake na kugundua kuwa kabla ya kutoa ngoma mpya ni lazima atafute kiki kupitia yeye jambo ambalo limemfanya kumdharau na kumuona kuwa ni msanii ambaye anapenya kwa kutumia mgongo wake.

Young Killer.

 

“Bila mimi yule bwana mdogo atakufa njaa, nimejaribu kumchunguza kila anapotaka kutoa ngoma mpya ni lazima atafute kiki kupitia mimi, iwe kwenye media ama kwenye mitandao ya kijamii, kwa hiyo kwa upande wangu naona jamaa hawezi kusimama mwenyewe,” alisema Dogo Janja a.k.a Janjaro.

Stori: Ally Katalambula | UWAZI SHOW-BIZ

Leave A Reply