The House of Favourite Newspapers

DOGO JANJA KATOA POVU KWA YOUNG DEE

0

JANJMSANII wa Hip Hop nchini Dogo Janja aliyekaa kimya juu ya kauli za Young Killer na Young Dee, sasa kafunguka na kusema Young Killer alimwambia  hamuwezi ni kwa sababu alishakuwa  role model wake, lakini alisema  hakupenda  Young Dee kumuita yeye ni kifaranga.

Alipoulizwa juu ya kauli ya Young Dee kumuita kifaranga, alifunguka: “Mimi pia sipendi kufananishwa na kifaranga japo sijakataa kufananishwa na Young Killer kwa sababu alishawahi kuwa role model wangu, kwa hiyo kufananishwa naye si  kitu kibaya, lakini kufananishwa na mla unga  Young Dee ndiyo sipendi tena mnakosea kabisa.

“Young Dee akiacha kula unga tutakaa mezani tuzungumze lakini kufananishwa naye sasa hivi sitaki kwani ni mtu ambaye ukimuacha nyumbani kwako unawaza vitu vyako kama TV, radio na vingine.  Je,  utavikuta salama,  maana asije kuiba kwenda kuuza,” alisema Dogo Janja

Hawa ni vijana wanaofanya vizuri kwenye muziki wa Hip Hop  nchini, ambako pia watu wanawafananisha kutokana na wote wanavyoimba kwa aina ya kurap ila kwa kila mmoja hapendi kufananishwa  na mwenziye.

NA : SAMSON JEREMIAH/GPL

Leave A Reply