DULLA: Makabila: Bifu Zinaua Singeli
MSANII wa Muziki wa Singeli, Dulla Makabila amefunguka kuwa muziki huo unakufa kwa sababu ya wasanii kuendekeza bifu za kishamba.
Akizungumza na Full Shangwe, Makabila alisema kuwa, licha ya Muziki wa Singeli kupiga hatua, wasanii wengi wamekuwa wakiendekeza bifu za hapa na pale.
“Singeli itakufa kwa sababu ya wasanii wake kuendekeza bifu za kipuuzi. Badala ya kusonga mbele, chuki na umimi ndiyo umetawala kwenye Singeli, mtu akifanya vizuri tayari watu wanaanzisha bifu, hatuwezi kufika jamani,” alisema.
STORI: MAYASA MARIWATA.