Abdul Sykes ‘Dully’
Ijumaa WIKIENDA:
MKONGWE asiyechuja kwenye gemu la Bongo Fleva, Abdul Sykes ‘Dully’ amewafungukia wasanii wanaoendelea kuamini kuwa kiki za mapenzi na mimba ni moja ya njia ya kukuza sanaa zao ni kufilisika kimawazo. Dully anayebamba na Ngoma ya Yono aliiambia Over Ze Weekend kuwa, anashangaa mlipuko wa kiki za mimba kwa sasa, kila msanii wa kike anaamini kiki nzuri ni kujisema kuwa ana mimba ya mtu fulani, hata baadhi ya wasanii wa kiume fahari kwao ni kusemwa ana uhusiano
Abdul Sykes ‘Dully’
USISAHAU na mtu fulani. “Binafsi naona ni kufilisika kimawazo, siamini katika ‘kujibrandi’ kwa mtindo huo, mfano mimi sitegemei kujianika maisha yangu binafsi ili nijulikane, sitegemei kuwa na uhusiano na watu maarufu ili jina langu liwe kubwa, wala sitegemei kutangazwa kwa namna yoyote ile ili niwe maarufu, mimi ni maarufu hata nisipojitangaza,” alisema Dully.
Stori: Ally Katalambula | IJUMAA WIKIENDA
Kwa stori zote kali, Tu-follow
Facebook @Globalpublishers
Twitter @GlobalHabari
Instagram @GlobalPublishers
YouTube @GlobalTVTZ
Endelea kutembelea website ya Global Publishers kila siku, tutaendelea kukusogezea kila news inayotokea mahali popote duniani.
Comments are closed.