ENGLAND YATOA KICHAPO KIKALI KOMBE LA DUNIA
Timu ya Taifa ya England leo Jumapili imefanikiwa kutinga hatua ya mtoano ya michuano ya Kombe la Dunia baada ya kuichapa Panama mabao 6-1 katika mchezo uliokuwa wa upande mmoja wa Kundi Ghuko Moscow, Urusi.
Kwa matokeo haya, England imefuzu hatua ya mtoano ya michuano hiyo huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi dhidi ya Ubelgiji ambao nao wamefuzu hatua inayofuata. Timu zingine zilizopo kwenye Kundi G ni Tunisia na Panama zenyewe zimeshatolewa kutokana na kutoshinda mchezo wowote, hawa watakutana kwenye mchezo wa mwisho wa kukamilisha ratiba.
Mashabiki wakishangilia wakiwa mitaani wakati wa mechi.
Comments are closed.