The House of Favourite Newspapers

EXCLUSIVE: Maisha ya Zabibu Kiba na Abdi Banda Sauzi – Video

Zabibu anaishi Polokwane, maisha yake yatakuwa hapa kwa kuwa mumewe, Abdi Banda anafanya kazi hapa. Anaichezea Baroka FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini. Timu nyingine mbili za Black Leopards na Polokwane City zinashiriki ligi hiyo na kuufanya mji huu kuwa na timu nyingi zaidi zinazoshiriki ligi kuu ya nchini hapa.

Zabibu ni kama Watanzania wengine na sasa maisha yake yamehamia katika mji huu ambao ni mwendo wa zaidi ya saa tatu na nusu kwa gari kutoka jijini Johannesburg.

Gazeti la Championi, limefanya mahojiano maalum na Zabibu akiwa nyumbani kwake mjini hapa na kueleza mengi.

Comments are closed.