The House of Favourite Newspapers

Fabregas: Fundi Wa Asisti Anayeacha Alama England

Cesc Fabregas

KIUNGO mahiri wa Chelsea , Cesc Fabregas anatazamiwa kuli­hama soka la Eng­land na bila shaka huenda ndio ikawa ndio kimoja, lakini anaondoka akiwa ameacha alama ya kuwa miongoni mwa mastaa walio­wahi kung’arisha ligi hiyo.

 

Fabregas, am­baye anata­z a m i w a k u ­jiun­g a na M o ­n a ­c o y a Ufaran­s a , atakum­b u k w a kwa sifa ya kama miongoni mwa mastaa wakali wa asisti.

 

Fabregas alianzia soka yake katika kituo cha kulelea yosso cha La Masia ambacho kinami­likiwa na Barcelona.

Akiwa na umri wa miaka 16 alichukuliwa na Arsenal na kuju­muishwa katika timu yao ya yos­so Septemba, 2003.

Kutokana na Arsenal kuka­biliwa na tatizo la majeruhi, alipenya katika kikosi cha kwanza cha Arsenal msimu wa 2004/05.

Alivunja rekodi nyingi za klabu ya Arsenal na mwaka 2005 alitwaa taji la Kombe la FA,

Hata hivyo, kutokana na kuwa na ndoto ya kuchezea timu yake ya utotoni, alion­doka Agosti, 2011 na kurudi Barcelona kwa uhamisho uliogharimu kiasi cha pauni milioni 35.

 

Alidumu Barcelona kwa miaka mitatu, ambako Fabregas akishiriki­ana na mastaa wen­gine Lionel Messi, Xavi Hernandez na Andres Iniesta alit­waa taji la La Liga, the Copa del Rey, Klabu Bingwa ya Dunia, UEFA Super Cup na mataji mawili ya Spain Super Cup.

 

Alirudi England mwaka 2014 lakini ingawa hakurejea Arsenal badala yake alijiunga na Chelsea kwa ada ya pauni mil­ioni 30, ambako katika msimu huo alisaidia timu hiyo kunyakua Kombe la Ligi na ubingwa wa Ligi Kuu England.

Kwa upande wa timu ya taifa, Fabregas alianza kuchezea His­pania mwaka 2006.

 

Pia alikuwemo kwenye kikosi kilichocheza Kombe la Dunia mwaka 2006, Euro 2008, Kombe la Mabara la FIFA 2009, Kombe la Dunia mwaka 2010, Euro 2012, Kombe la Mabara 2013, Kombe l a Dunia 2014 na Euro 2016.

Alitoa mchango mkubwa kwa Hispania kutwaa mataji Ulaya ka­tika miaka yaani 2008 na 2012 na mafanikio ya kutwaa Kombe la Dunia 2010, ambapo alitoa pasi kwa Andres Iniesta kufunga bao la ushindi kwenye mechi ya fainali.

 

Fabregas enzi zake akiwa kwenye kiwango alikuwa kivutio kumtazama kutokana na umahiri wake wa kupiga chenga, kutoa pasi na kufunga ma­bao.

Staa huyo alikuwa na kipaji binafsi lakini mafanikio yake ni matunda ya kunolewa na kituo cha kulelea yosso cha La Masia ambacho kinamilikiwa na klabu ya Barcelona.

 

Fabregas ana uwezo wa kucheza nafasi yoyote katika kiungo lakini pia anamudu kucheza kama straika.

Makali ya Fabregas yanathibi­tishwa kuwa ni staa namba mbili mwenye asisti nyingi zaidi kwenye Ligi Kuu England akiwa ametoa 111 akiwa nyuma ya mastaa kama Ryan Giggs na kuwazidi nyota kama Frank Lampard, Dennis Bergkamp, Steven Gerrard na David Beckham.

 

Fabregas pia ana sifa ny­ingine ya kucheza kwa ari na pia haogopi na tabia hizo na alikuwa anazo tangu akiwa mdogo.

M a t h a l a n i aliwahi kui­fungia Arse­nal kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Barcelo­na mwaka 2010 wakati akiwa ame­vunjika mguu.

 

Pamoja na kuwa Fabregas ali­chezea timu ambazo zilikuwa na wachezaji mahiri lakini mara zote nyota yake iling’ara pia.

Ingawa kuna baadhi ya watu wamekuwa wanamponda kuwa eti alikuwa akipata msaada mkubwa na hasa alipokuwa kwenye timu za Bar­celona, na Chelsea.

 

Hata hivyo, Fabregas alikuwa mkali kwani ukiangalia akiwa Arse­nal alipewa unahodha akiwa na umri mdogo lakini pia aliiongoza timu hiyo ikiwa haina fungu kubwa la kusajili mastaa kutokana na kulipa deni la ujenzi la Uwanja wa Emirates.

 

Fabregas alikuwa anaiongoza Ar­senal katika kipindi ambacho ilikuwa imewapoteza mastaa kama Thierry Henry, Patrick Vieira na wengineo, ambao ndio walikuwa chachu ya kikosi cha kutisha cha Arsenal kili­chomaliza Ligi Kuu England bila ya kupoteza mechi msimu wa 2003/04.

LONDON, England.

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.