Gladness Kifaluka Ajipa Umalkia
KOMEDIANI matata wa kike Bongo, Gladness Kifaluka ‘Pili Kitimtim’ anasema kuwa kwa wasanii wa kike wa uchekehaji Bongo, yeye ndiye umalkia kamili.
Akistorisha na IJUMAA SHOWBIZ,Galadness anasema hakuna komediani wa kike ambaye anaweza kumfikia hata robo kwenye uchekeshaji.
“Mimi ndiye msanii wa kike kwenye uchekeshaji, anayebisha aje tushindane, kwa mambo ninayoyafanya kwa sasa hivi kwenye hii tasnia naweza nikasema mimi ndiye malkia,” anasema Gladness na kusisitiza kwamba leo atakiwasha kwenye Jukwaa la Cheka Tu pale Mlimani City.