Kamanda Sirro akizungumza na wanahabari leo
Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro amesema kati ya watuhumiwa hao .
Baadhi ya madawa ya kulevya yaliyokamatwa na polisi.
Wamo wauzaji, wasafirishaji na watumiaji wa dawa za kulevya, na kwamba wataanza kufikishwa mahakamani siku ya kesho, huku mmoja akipandishwa kizimbani leo.
Kijana Omary Abeid Bakari anayedaiwa kutaja majina feki ya vigogo watumia unga.
Pia ametoa taarifa ya kijana Omary Abeid Bakari anayedaiwa kusambaza taarifa za uongo, ambapo amesema kuwa jeshi hilo linamshikilia kijana huyo ambaye ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23, anayedaiwa kutaja majina ya viongozi na kuwatuhumu kuwa wanahusika na dawa na dawa za kulevya.
Kamanda Sirro amesema hadi sasa jumla ya kete 612 pamoja na bangi vimekamatwa na kwamba kuna watu wengine 17 ambao bado jeshi hilo linawafuatilia na watakuwa mbaroni wakati wowote.
PICHA ZOTE NA DENIS MTIMA | GLOBAL PUBLISHERS
Comments are closed.