Wananchi Wasisitizwa Kutunza Vyanzo Vya Maji
Mwananchi wasisitizwa kulinda vyanzo vya maji
Bodi ya maji Bonde la Wami Ruvu imeendelea kusisitiza wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji kwa kuzingatia Sheria za mita sitini
Wito huo umetolewa na mwanasheria bodi ya maji Bonde la Wami Ruvu Aloyce Lyimo wakati akizungumza jukwa la wadau wa maji wa kidakio cha Wami ambapo amesema licha ya elimu kutolewa bado kumekua ya uharibifu na uvamizi wa vyanzo vya maji
Amesema suala la kutunza vyanzo vya maji ni jukumu la kila la mtu sio la Bode la Wami peke yake hivyo watendaji wa vijiji na wenyeviti wanatakiwa kutoa elimu kwa wananch
Akizungumza katika jukwa Hilo kaimu ya Maji Wami Ruvu Mhandisi Amy Mchele amesema kuwa ina imani kubwa na Jukwaa la Wadau Kidakio Cha Wami litakuwa na uwezo wa kupambana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika kidakio hic
Mhandisi Amy amesema kuwa wadau hao wanajukumu la Kuandaa mikakati thabiti katika kulinda rasilimali za maji ikiwemo usimamizi wa sheria,utekelezaji wake pamoja na kutoa elimu
Kwa upande wa Mwanasheria kutoka Bodi ya maji Bonde la Wami/ Ruvu Bw. Aloyce Lyimo amesema kuwa undwaji wa kamati hiyo umefanyika kwa njia ya ushirikishwaji ambapo majina ya wajumbe yamependekezwa na Wadau wallohudhuria kwenye jukwaa
baadae kupelekwa kwenye Bodi na wajumbe kuanza kazi mara baada ya Kupendekezwa, namuhoi.i. ezwa,