Global yagawa nailoni kwa wauzaji wa Magazeti Dar
Maofisa wa Global Publishers Kitengo cha Usambazaji, Jordan Ngowi na Jimy Haroub (walioko mbele) wakimwekea muuzaji wa magazeti jinsi ya kufunika magazeti kwa nailoni ili yasilowe eneo la Kituo cha Daladala cha Mwenge, Dar.
Muuzaji wa Magazeti Kituo cha Lufungira-Mwenge (kushoto ) akisaidiwa kufunika nailoni kwenye meza yake ya magazeti ili yasilowe, anayelekekeza ni Jordan Ngowi.
Baadhi ya wauzaji wa magazeti maeneo ya mataa ya Ubungo wakipewa nailoni kwa ajili ya kufunika magazeti.
Muuzaji wa magazeti eneo la kituo cha daladala cha Kimara-Baruti (mwanamama aliyeko katikati) akisaidiwa kuweka nailoni kutoka kwa maofisa usambazaji wa Global.
Muuzaji wa magazeti eneo la Malamba Mawili -Mbezi akifurahia mara baada ya kuelekezwa jinsi ya kutumia nailoni kufunikia magazeti aliyokuwa akiyauza.
Ofisa usambaziji, Jimy Haroub (kulia) akimuelekeza muuza magazeti jinsi ya kufunika nailoni meza yake ya magazeti ili yasilowe.
Muuzaji wa magazeti eneo la kituo cha daladala cha Kinyerezi (kulia) akisaidiana na Jimmy Haroub wa Global kufunika magazeti kwa nailoni.
MAOFISA usambazaji wa Kampuni ya Global Publishers Ltd ambao ni wachapishaji wa Magazeti ya Uwazi, Championi, Amani, Risasi na Ijumaa leo wamegawa nailoni maalim kwa ajili ya kufunikia magazeti wakati wa mvua kwa baadhi ya wauzaji wa magaeti jijini Dar es Salaam.
Maofisa hao ambao wamefanya zoezi hilo la kugawa nailon hizo waliongozwa na Jordan Ngowi akisaidiwa na Jimy Haroub ambao wameweza kuzunguka maeneo tofauti jijini kwa ajili ya utoaji wa nailoni hizo.
Lengo la kugawa nailoni hizo ni kuwawezesha wauzaji wa magazeti kuuza hata kipindi mvua kutokana na msimu wa mvua za vuli kuanza jijini Dar.
NA DENIS MTIMA/GPL