The House of Favourite Newspapers

Gymkhana Yasherekea Miaka 100 Ya Kuanzishwa Kwake Kwa Mtindo Wa Kipekee

0

Mwenyekiti wa klabu ya Dar es salaam Gymkhana, Walter Chipeta (kulia) akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es salaam. Klabu hiyo iko mbioni kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1916 ambapo imejipanga kuandaa michuano ya michezo mbalimbali kama Gofu, Kriketi, Tenisi, Skwashi, Soka, mchezo wa kuogelea na mingine mingi inayotarajiwa kuanza Julai 03 na kuhitimishwa Julai 08. Katikati ni Meneja Msaidizi wa klabu hiyo, Elizabeth Michael na kushoto ni Mratibu wa Masoko na Matukio Levina George.

Mwenyekiti wa klabu ya Dar es salaam Gymkhana, Walter Chipeta (kushoto)  akiwaeleza waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam kuhusiana na dhamira ya klabu hiyo ya kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1916. Klabu imejipanga kuandaa michuano ya michezo mbalimbali kama Gofu, Kriketi, Tenisi, Skwashi, Soka, mchezo wa kuogelea na mingine mingi inayotarajiwa kuanza Julai 03 na kuhitimishwa tarehe Julai 08 katika kuadhimisha siku hiyo ya kihistoria. Kulia ni Meneja wa Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Ndugu Itandula Gambalagi.
Meneja wa Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Ndugu Itandula Gambalagi akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusiana na udhamini wa mashindano yatakayosindikiza maadhimisho ya miaka 100 ya klabu ya Dar es Salaam Gymkhana tangu ilipoanzishwa mwaka 1916. Katika kuadhimisha siku hiyo ya kihistoria, klabu imejipanga kuandaa michuano ya michezo mbalimbali kama Gofu, Kriketi, Tenisi, Skwashi, Soka, mchezo wa kuogelea na mingine mingi inayotarajiwa kuanza Julai 03 na kuhitimishwa tarehe Julai 08.Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ndio mdhamini Mkuu wa mashindano hayo. Wadhamini wengine wa mashindano hayo ni pamoja na Clouds Media Group, Qatar Airways, ALAF, GSM, Serena Hotel, Eagle Africa Insurance brokers, Vodacom na Mwananchi Communications.Kushoto ni Mwenyekiti wa klabu ya Dar es salaam Gymkhana, Walter Chipeta.
Mwenyekiti wa klabu ya Dar es salaam Gymkhana, Walter Chipeta akisalimiana na Meneja wa Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Ndugu Itandula Gambalagi wakati wa mkutano wa waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam. Klabu hiyo iko mbioni kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1916 ambapo imejipanga kuandaa michuano ya michezo mbalimbali kama Gofu, Kriketi, Tenisi, Skwashi, Soka, mchezo wa kuogelea na mingine mingi inayotarajiwa kuanza Julai 03 na kuhitimishwa tarehe Julai 08. 

Dar es Salaam.  Klabu ya , Dar es Salaam Gymkhana Club (DGC) itasherekea kutimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake  kwa kufanyika mashindano ya michezo ya aina mbalimbali kuanza Julai 3 na kumalizikia Julai 8 .

Mwenyekiti wa DGC, Walter Chipeta alisema kusherehekea kutimiza miaka 100 kwa staili ya tofauti tangu kuanzishwa kwake mwaka 1916.

Miongoni michezo iliyopangwa kufanyika katika kuadhimisha miaka 100 ya klabu hayo ni pamoja na gofu, tenisi, skwashi, soka, kriketi, mchezo wa kuogelea na mingine mingi ambayo kwa ujumla itawahusisha wanachama na wasio wanachama wa klabu hiyo.

Mashindano hayo yamedhaminiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Mwananchi Communication Ltd, Hotel ya Serena, Clouds media group, Qatar airways, GSM, na  Eco Africa.

Chipeta amesema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na klabu kadhaa zimethibitisha kushiriki katika mashindano hayo ambayo pia yataambatana na tafrija maalum ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga chumba kwenye taasisi ya ugonjwa wa Saratani ya Ocean Road.

“Tunatarajia kuwa na michezo yenye kusisimua sana mashabiki, mbali ya soka ambayo itashirikisha timu mbalimbali, wachezaji wa gofu maarufu wa Afrika Mashariki nao watashiriki katika mashindano hayo ambapo washindi watazawadiwa zawadi mbalimbali,” alisema Chipeta.

Menaja Mauzo wa NHC, Itandula Gambalagi alisema kuwa wamemua kudhakini maadhimisho hayo kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya michezo nchini kwani klabu ya Gymkhana ina michezo mbalimbali kwa ajili ya maendeleo nchi.

“Hii ni faraja kwetu, kwa kushiriki katika maadhimisho haya, tutaweza kusaidia wachezaji wa tenisi, gofu, skwashi na kuogelea, tunaomba wadhamini wajitokeze ili kufanikisha miaka 100 ya klabu hii,” alisema  Gambalagi.

Leave A Reply