The House of Favourite Newspapers

Futuru Bure na Nikohub

0

HABARI ya mjini kwa sasa ni hii, ambayo imeingizwa na Kampuni ya Nikohub, inayokuwezesha mtu yoyote mahali ulipo kuweza kufuturu bure kwenye mwezi huu wa Ramadhani.

Kampuni ya Nikohub, inakuwa ya kwanza nchini kuungana na Waislamu wote kwenye mwezi huu Mtukufu wa Mfungo wa Ramadhani, ambapo kwa kuzingatia umuhimu wa kila mmoja aliye kwenye mfungo huo, kushiriki naye kwa kumuwezesha kupata futari bure popote pale alipo.

“Kufuatia ukuaji wa mfumo wa Sayansi na Teknorojia hapa nchini, Nikohub tunakuwezesha kufuturu mahali popote endapo tu utaweza kujiunga nasi kwa ku-download App yetu ya Nikohub, kwenye simu yako. App hiyo ipo kwenye play store, ukishaidownload, jiunge ili uonekane moja kwa moja kwenye ‘system’ ya Nikohub.

“Ukimaliza hivyo vyote, unatakiwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno ‘SMS’ au tupigie simu namba 0765-80 24 57, ili uweze kupata maelekezo ya jinsi ya kufuturu bure popote pale utakapokuwa kwa muda huo.

“Kumbuka kujiunga kwako na App ya Nikohub, utaweza kuwa mmoja kati ya watu 100 ambao kila siku tumekuwa tukiwafuturisha bure.”

Leave A Reply