The House of Favourite Newspapers

Harusi ya Sugu inavyomtesa Faiza!

SHUGHULI ya harusi yake aliyoitangaza Mbunge wa Mbeya-Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ inamtesa kinoma mzazi mwenzake, Faiza Ally, kiasi cha kusitishe safari ya kurudi Bongo hadi shughuli hiyo ipite.  Akizungumza kwa WhatsApp na Gazeti la Ijumaa Wikikenda, Faiza alisisitiza kuwa hakuna asiyejua ni jinsi gani anampenda Sugu hivyo ameamua kujipotezea na kazi zake mpaka harusi ipite.

“Kwani hata wewe mwandishi hujui kuwa ninampenda Sugu? Kiukweli ninaumia sana kwa sababu siwezi kupenda mwanaume hapa duniani kama yule, ngoja nijizubaishe huku China, nifanye kazi za watu hadi harusi iishe ndiyo nitarudi Bongo, sitaki stresi mimi,” alisema Faiza aliyezaa mtoto mmoja na Sugu huku akisisitiza kuwa hata kama ameoa, bado anampenda

Comments are closed.