The House of Favourite Newspapers

Huyu Ndiye kinara wa Matokeo Kidato cha Nne

Mwalimu wa Feza Boys, Ismail Nguno akifanya mahojiano na Gloal TV Online na mtandao wa Global Publishers.

 

BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA), limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2017, ambapo ufaulu umepanda kwa asilimia 7.22 huku watahiniwa 265 wakifutiwa matokeo kwa udanganyifu.

 

Fuad Thabit katika pozi.
…Akipiga picha ya pamoja na mtangazaji wa Global TV Online, Catherine Kahabi.

 

Baada ya matokeo hayo kutangazwa na Katibu Mtendaji wa Necta, dkt. Charles Msonde, Global Publishers imefunga safari hadi Kunduchi jijini dar es Salaam ambapoilipo Shule ya Sekondari feza Boys ambayo imeshika nafasi ya pili Kitaifa na imetoa mwanafunzi wa sita Kitaifa katika matokeo hayo.

Baada ya kuwasili shuleni hapo tumebahatika kuonana na kufanya mahojiano na kinara huyo ambaye ni Fuad Thabit Thabit (17) ambaye ameeleza furaha yake kufuatia ushindi huo wa kihistoria kwake.

 

“Ninamshukuru Mungu kwa kuniwezesha kupata matokeo haya. Jambo kubwa nililokuwa nikilifanya darasani ni kuwasikiliza vyema walimu wangu, kufanya juhudi na bidii zaidi katika masomo yangu, lakini kikubwa zaidi nilikuwa nikimtegemea Mwenyezi Mungu, niliamini na ninaamini ni Mungu pekee ndiye amebifanya niweze kufikia hapa niliopifika leo.

Wanafunzi wenzake wakimbeba kwa furaha kutokana na ushindi huo.

 

“Vile vile wazazi walikuwa ni nguzo kubwa kwangu katika kunitimizia mahitaji yangu ya shule, kunitia moyo na kunihimiza kuenenda katika maadili mema,” alisema Thabit.

Katika picha ya pamoja na mtangazaji wa Global TV.

 

Orodha ya Shule 10 Bora.

1. St. Francis Girls – Mbeya
2. Feza Boys – Dar es Salaam
3. Kemoboya – Kagera
4. Bethel Sabs Girls – Iringa
5. Anwarite Girls – Kilimanjaro
6. Marian Girls – Pwani

7. Canossa – Dar

8. Feza Girls – Dar

9. Marian Boys – Pwani

10. Shamsiye Boys – Dar

Mwalimu Ismail akimpongeza mwanafunzi wake .

 

Shule Kumi (10) Za Mwisho Kitaifa

1. Kusini – Kusini Unguja

2. Pwani Mchangani – Kaskazini Unguja

3. Mwenge SMZ – Mjini Magharibi

4. Langoni – Mjini Magharibi

5. Furaha – Dar

6. Mbesa – Ruvuma

7. Kabugaro – Kagera

8. Chokocho- Kusini Pemba

9. Nyeburu – Dar

10. Mtule – Kusini Unguja

 

Majengo ya Feza Boys.

PICHA NA DENIS MTIMA | GPL

 

Global Publishers App imekurahisishia kutazama matokeo ya kidato cha nne kupitia simu ya mkononi. Install Global Publishers sasa uyasome yote: Bofya  au 

Comments are closed.