LEBO mpya ya muziki wa ya Instincts Records iliyopo Kinondoni-Studio jijini Dar jana imefanya uzinduzi wa lebo hiyo itakayosimamia kazi za wasanii wa Kibongo kwa levo za kimataifa na kuzindua video ya ‘Falling in Love’ ya msanii Shose Modest ‘Shose’ ambaye ameanza kusimamiwa na kampuni hiyo.
Uzinduzi huo umefanyika katika Hoteli ya Regency Park Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo wadau na wasanii mbalimbali walihudhuria kushuhudia uzinduzi huo, ulioambatana na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.
Akizungumza na mtandao huu Mkurugenzi wa Lebo ya Instincts Records, Joseph Mwanukuzi, alisema kuwa wamejipanga kufanya mabadiliko ya kuwasimamia vizuri wasanii na kuwafanya wanufaike na kazi zao.
“Lengo letu ni mabadiliko ya sanaa nchini, wasanii wanufaike kama ilivyo kwa wasanii wa mataifa mengine, kwa kuanza tunamsimamia Shose, na kila mwaka tutakuwa tunawasaini wasanii wanne, ambao wana nidhamu ya kazi, wanajituma na wana kipaji, hivyo ndiyo vigezo vyetu,” alisema Mwanukuzi.
Baadhi ya wasanii waliohudhuria katika uzinduzi wa lebo hiyo ni Country Boy, Izzo B, Bella, Mchizi Mox, One Incredible na wengineo.
PICHA STORI: DENIS MTIMA NA GABRIEL NG’OSHA/GPL
Comments are closed.