ISHA MASHAUZI ALIVYOSHEREHEKEA BETHDEI NA WANAFUNZI
Muimbaji wa taarab na Mkurugenzi wa Kundi la Mashauzi Classic, Isha Ramadhani Makongo maarufu kama Isha Mashauzi leo amesherehekea siku yake ya kuzaliwa na wanafunzi wa shule ya Msingi Mnazi Mmoja ambayo alisoma.
Katika sherehe hiyo Isha aliongea na wanafunzi hao kisha akalishana nao keki kama ilivyo kawaida.
Baada ya hafla hiyo Isha amesema ameamua kuifanyia bethdei hiyo shule hapo kutokana na maarifa mengi aliyoyapata akiwa mwanafunzi wa shule hiyo aliyosoma kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari.
PICHA/HABARI: RICHARD BUKOS | GPL
Comments are closed.