Jaji Mkuu wa Kenya ashinda tuzo ya kiongozi bora wa kike wa Mwaka barani Afrika 2023
Jaji Mkuu wa Kenya Martha Koome ametunukiwa tuzo ya Kiongozi Bora wa Kike wa Mwaka wa Afrika 2023 wakati wa hafla iliyofanyika Addis Ababa, Ethiopia.
Katika hotuba yake ya kukubali tuzo hiyo, bi Koome alisema kuwa utambuzi huo uliashiria kujitolea kwa pamoja na uthabiti wa watu binafsi wanaojitahidi kupata ubora katika bara zima.
“Tuzo hii sio yangu peke yangu. Ni sifa ninayojitolea kwa moyo wote kwa taasisi niliyobahatika kuongoza, Idara ya Mahakama ya Kenya,” Koome alisema.
“Kutambuliwa huku kunatuchochea kuendelea kutafuta uongozi bora na kuongeza bila kuchoka ubora wa utoaji wa huduma kwa taasisi zetu,” Koome alisema.
Wakati huo huo Rais Mstaafu wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete alitunukiwa tuzo ya kiongozi bora kwa mwaka 2023 katika upande wa amani na usalama wa bara la Afrika.