The House of Favourite Newspapers

Jamani Antiii…Nishushe Ununio..!-15

ILIPOISHIA RISASI MCHANGANYIKO:

Hata hivyo, kabla Bigambo hajasema chochote kutokana na kauli ya Vivian alimimina tena ‘nyagi’ kwenye glasi na kuipiga yote kabla ya kumimina tena na kuiweka mezani bila kuinywa na hapohapo akanyanyuka kidogo na kujiweka sawa ambapo sasa aligeukiana na Vivian, alimtazama usoni na wote wakawa wametazamana bila kupepesa macho na Bigambo akapanua mdomo kama anayetaka kuuliza kitu kwa staili ya kipekee.

“Sawa, tuendelee kuwa kwenye mahusiano na mimi kukufurahisha wewe ni sehemu ya kazi yangu,” Bigambo alisema huku akikamata glasi na kujimiminia kwa kasi huku akikunja ndita, uchungu wa nyagi uliendelea kulipa kazi ya ziada koromeo lake.

Vivian alikaa kimya kwa muda. Kabla hajasema lolote, alikamata chupa ya reds na kujimiminia kama alivyofanya Bigambo. Walikaa kimya kwa muda kabla ya kuendelea na mazungumzo.

Kuona kama Bigambo anamchelewesha, Vivian alimsogelea na kuanza kumpa uchokozi wa wazi kabisa ulioashiria kwamba anataka dozi ya maana kwa wakati huo na siyo maneno mengi kama ilivyokuwa wakati wakiwa nje.

“Baby,” Vivian aliita kwa sauti kavu lakini yenye kuelemewa na mahaba mazito sana.

“Mmmh,” Bigambo aliitika lakini kabla hajafanya chochote alishangaa kumuona Vivian akichukua nguo na kuanza kuvaa huku akitokwa na machozi. GALAGALA NAYO SASA…

BIGHAMBO aliruka kama kima kwenye miti ya mvinje na kumshika Vivian huku akimuuliza kulikoni aanze kulia baada ya kutoka kwenye gwaride la kupeana raha za kidunia.

“Mbona unakuwa hivyo jamani?” Bigambo aliuliza huku akimshika kwa uangalifu wa hali ya juu sana, Vivian akajisikia amani moyoni na kuamua kuachana na zoezi la kuvaa na sasa akasimama wima na Bigambo, wote wawili wakajikuta wamekaribiana na kugusana tena.

Joto la miili yao lilikuwa limepanda na kufikia kiwango ambacho kama ni mgonjwa wa malaria hali ilikuwa mbaya sana. Wote walibaki kama walivyokuja duniani na Bigambo alimfuata Vivian na kumvaa mzimamzima na wote waliangukia kitandani puuu…

Bigambo alipeleka kinywa hadi kwenye papi za mdomo wa Vivian, ambaye midomo yake ilikuwa na lipsi nene na zenye kuvutia zaidi. Vivian alilala kwa mtindo wa kuhesabu mabati. Bigambo kuona hivyo, akiongozwa na mhemko wa kilevi alichokuwa ameshindilia ubongoni, alianza kuyakabili matunda ya mwanamke huyo ambaye kwa wakati huo alikuwa akihema kama bata dume aliyetoka kupambana na jogoo.

Hakuishia hapo. Bigambo alianza kufanya utalii kwenye maeneo mbalimbali ya mwili wa Vivian aliyekuwa akiendelea na kuhema huku akifumba na kufumbua macho. Ili kuwa ni raha isiyoelezeka.

Vivian aliendela kujitikisa kwa kufuatisha msisimko uliotokana na utalii wa Bigambo mwilini mwake. Hakika Bigambo alikuwa mtaalam wa mahaba, raha aliyompa Vivian ilikuwa haina kifani. Raha hiyo ilimfanya Vivian ashindwe kujizuia na kuanza kuropoka maneno mengi ya hovyo.

“Bigambo…”

“Naam…”

“Unajua sana jamani baba.”

“Kufanya nini?”

“Kunipa raha,” Vivian alijieleza kwa maneno yote matamu aliyoyajua lakini Bigambo hakusitisha suluba zake ambapo sasa alianza kutumia jembe lake kumuadhibu Vivian. Kwa kifupi wote walizama kwenye dimbwi la mahaba.

Mtanange ulikuwa wa kukata na shoka. Timu zote mbili zilikuwa zikishambulia lango la timu pinzani kwa nguvu na pasi za kushtukiza. Ikafika mahali Vivian alichoka na kuruhusu mashuti kadhaa yatikise nyavu.

Muda mfupi baadaye, wote wawili walijikuta wakitangaza kufika mwisho wa miti ya minazi na sasa walialikana kupasua madafu pamoja. Kwa upande wa Bigambo lilikuwa dafu lake la kwanza kupasua tangu waanze kazi ya kukwea minazi lakini kwa upande wa Vivian lilikuwa kama dafu la nne.

“Nafika…,” Vivian alianza kutangaza kwa sauti ya kupayuka huku akihangaika mwili mzima ili ashike vizuri asije akaanguka na badala ya kuvunja dafu iwe stori nyingine.

“Umefika wapi mama…?” Bigambo alihoji lakini kabla hajajibiwa naye alianza kusikia kitu cha tofauti na sasa alianza kukoroma huku akikunja sura na hapohapo alianza kuropoka kwa sauti yake ile mbaya.

“Oooh, mama nami naelekea kupasua daaaafuuuu…,” Bigambo aligugumia na hapohapo alizidisha kasi ya ukweaji na kulishika dafu moja kabla ya kuliachilia na kulipasua kwa hasira kali, kitendo kilichomfanya Vivian naye apasue la kwake wote kwa pamoja walijikuta wakihitimisha safari kwa wakati mmoja, lakini kufumba na kufumbua Vivian alianza kuonesha jambo ambalo hata Bigambo lilimshangaza kwani hakulitegemea.

Bigambo alijivika ustaarabu ambao hakuwa nao na lengo likiwa ni kumpumbaza Vivian, ili atoe ushirikiano ambao ungeleta matokeo chanya kwa mpambano huo wa watani wa jadi.

Bigambo alimfuata Vivian mahali alipokuwa amelala na kuanza kumfanyia fujo zote ambazo hufanyiana wapendanao pindi wanapokutana kwenye eneo walilokuwepo Bigambo na Vivian.

Vivian naye alimpokea na safari hii alilala kwa mtindo wa kawaida, aliweka kichwa maeneo ya kiuno na akawa kama anakibilingisha kichwa, hali iliyopelekea hali ya Bigambo kuanza kubadilika.

Vivian hakuishia hapo, akajisogeza kwa mbele zaidi na wote wawili kujikuta wakitazamana usoni.

“Baby…” aliita Vivian wakati huohuo mkono wake wa kushoto ukitalii kwa umaridadi mkubwa kabisa kwenye vichuguu vifupi viwili, mahali ambapo maruhani ya Bigambo yalikuwa.

“Mmm…,” aliguna Bigambo kwa mtindo wa kufyonza muwa mtamu…

“Oooh, yes baby…,” Vivian alichombeza kwa maneno laini na kuyafumba macho kwa maana ya kuhamasisha zaidi. Hali ya Bigambo ikazidi kuwa mbaya, kama ni kuharibikiwa sasa ilikuwa kwa kiwango cha kuhitaji msaada kamili na si maneno matupu.

Kuona hivyo, Vivian akazidisha mbwembwe. Akafumba macho na kukisogeza kinywa karibu na kile cha Bigambo. Bigambo naye akalegea kwa maana ya kumpokea Vivian kwa mtindo huo. Wakasogeleana na kuanza kushiriki pamoja kutafuna miwa ya Kilombero.

Walifanya hivyo kwa muda wa zaidi ya dakika kumi na tano, kila mmoja akionesha ufundi wa namna ambayo miwa mitamu huliwa.

Vivian alizidisha manjonjo, akawa anajikunja kwa kuweweseka kimahaba zaidi, ikawa mara akunje miguu na wakati mwingine ainyooshe kama anayejipima urefu, ilimradi kuonesha namna ambavyo alikuwa amekolea kwenye dimbwi la uhondo wa kilichokuwa kikiendelea.

Bigambo hakuwa nyuma. Naye aliamua kupeleka mashambulizi kwa Vivian, tena yalikuwa yale ya kushtukiza kwa lengo la kumvizia adui akiwa amejisahau.

Bigambo alipeleka mkono mmoja na kuyavamia maembe bolibo ya Vivian na kuyashika kama anataka kuhakikisha yameiva au la…

Hakuishia hapo, akalishika embe moja na kulitupia mdomoni huku lile jingine akiendelea kulifanyia visa vya kichokozi… Vivian akashindwa kuvumilia.

Sasa akajiachia kwa uhuru, akakaa mkao ambao ulimpa uhuru Bigambo kuonesha utundu wake zaidi ya huo. Kuona hivyo, Bigambo akaona isiwe tabu zaidi ya kupania kuonesha ufundi maridhawa, akamfuata Vivian na kumuweka vyema.

Kufikia hapo, Vivian alikubali kutoka moyoni kabisa kwamba Bigambo ni mtaalam kwenye eneo la kusakata kabumbu hususan kama mechi yenyewe imewakutanisha watani wa jadi ambao kila mmoja hutazama sana ushindi wa pointi na si wingi wa vyenga kama ambavyo wengi hudhani.

Walicheza ligwaride hadi kila mmoja akaridhika na mwisho wa siku wakakubaliana kuondoka eneo hilo kwa kuwa Vivian alikuwa na ratiba ya kukutana na mtu nyumbani kwake, huku Bigambo akitarajia kwenda kufanya kazi zake binafsi.

“Lakini baby,” Vivian alisema huku akitafuta mahali zilipokuwa nguo zake.

“Vipi mama.”

“Wewe ni kiboko.”

“Kwa nini?”

“Si kama hivi, kwanza sikuwa na mpango kabisa wa kufanya chochote tena na usingeniwahi wakati navaa, ndiyo kwanza ningekuwa nimeshafika nyumbani zamani mno, lakini uungwana wako wa kuniwahi na kunibembeleza kwa maneno na bembelezo maridhawa, hatimaye tumeweza kurudia mchezo tena,” Vivian alisema huku akimtazama Bigambo kwa lile jicho la pembeni na kuachia tabasamu laini.

“Umetumia utundu wako wote kuhakikisha najikuta nikiingia mchezoni tena, hakika umeniweza.”

“Kwa hiyo umecheza gemu kwa kulazimishwa?”

“Sijamanisha hivyo bwana.”

“Sasa kumbe?”

“Mwanzoni sikutaka kwa kweli, lakini ushawishi wako umesaidia sana hadi nikajikuta nafurahia maandalizi na hatimaye namna ambavyo mchezo mzima ulivyokwenda,” Vivian alisema na hapohapo akawa anamalizia zoezi la kuvaa na kumsubiri Bigambo amalize ili waweze kutoka pamoja kabla ya kuachana na kila mmoja kuangalia njia na ratiba yake.

Kwa maoni na ushauri nicheki kwa namba hizi;

0679-659 633.

Comments are closed.