The House of Favourite Newspapers

Jini Kabula Aanika Siri ya Kunawiri Kwake

BAADA ya mwaka jana kuugua na kwenda kupumzika kwao Mwanza na sasa kuonekana kuwa na hali nzuri, msanii wa filamu za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ ameibuka na kuanika siri ya kunawiri kwake.

 

Akipiga stori na Za Motomoto News, Jini Kabula alisema kunawiri kwake kunatokana na kupumzika kwa miezi mitatu bila mikikimikiki huku akila vinono nyumbani kwa kaka yake alikoenda kwa mapumziko na hivi karibuni ana mpango wa kurejea tena Dar kwa ajili ya kufanya biashara ili kujiendeshea maisha na siyo sanaa tena kwa sasa.

 

“Jamani kunawiri kwangu ni kwamba ninakula vinono kwa kaka yangu huku Mwanza, sina stress maisha yanaenda tu vizuri, nimeshapumzika miezi mitatu kama daktari alivyoshauri na ninajiandaa kurudi kwa ajili ya mishe nyingine za kimaisha,” alisema Jini Kabula.

Comments are closed.