The House of Favourite Newspapers

Jinsi ya kujikinga na magonjwa

0

brunette sitting down and stretching her legs on white backgroundKuna njia nyingi ya kujikinga na magonjwa mbalimbali hasa yale ya kuambukiza au kuambukizwa.

Moja ya ugonjwa hatari duniani na ambao huua watu wengi ni malaria.

Ugonjwa huu huenezwa na mbu. Ili kujikinga na ugonjwa huu watu  wanashauriwa wawe wakihakikisha wanaharibu maeneo ambapo mbu huzaliana.

Wanashauri wa kufunika matangi ya maji na beseni za kufulia nguo. Kuharibu vyombo vyote vya kutekea maji ambavyo havina mifuniko.

Watu wanaelekezwa na wasiache maji katika vyombo vya kuwekea maua kwani mbu wanaweza kutaga mayai katika maji ya madimbwi hayo na kuzaliana kisha mbu hao kung’ata watu na kuugua malaria.

Epuka kuwa nje wakati wadudu wengi wanapoanza kutokea, vyandarua na vitumike.

Epuka kuwa karibu na mifugo mara nyingi kwani unaweza kuambukizwa ugonjwa iwapo utaumwa na wadudu waliowauma mifugo hao.

Washiriki wote wa familia wanapaswa kutumia vyandarua hasa vilivyotiwa dawa ya kuwafukuza wadudu, weka nyavu madirishani na uzitengeneze zinapoharibika,  ziba nyufa zilizo pembeni mwa paa la nyumba ambapo wadudu wanaweza kuingia.

Njia hizo za kujikinga zinagharimu kiasi fulani cha fedha, lakini unaweza kupoteza fedha nyingi sana ikiwa utalazimika kumpeleka mtoto hospitalini au mtu anayetegemewa katika familia pale anapougua.

Wazuie wadudu wasijifiche mahali popote nyumbani mwako. Piga lipu ukutani na kwenye dari na uzibe nyufa na mashimo. Ikiwa nyumba imeezekwa kwa nyasi funika dari kwa kitambaa cha kuwazuia wadudu.

Ondoa vitu vilivyorundikana kama vile karatasi, nguo au picha nyingi zilizowekwa ukutani, kwani huko ndiko wadudu hujificha.

Usiwakaribishe kamwe panya na wadudu, tumia dawa za kuwafukuza na za kuwaua, lakini usisahau kufuata maagizo yaliyoonyeshwa.

Tumia mitego ya inzi na vifaa vya kuwaua, uwe mbunifu; mwanamke mmoja alitumia kitambaa kutengeneza mifuko, kisha akajaza mchanga katika mfuko huo na akauweka chini ya mlango ili kuwazuia wadudu wasiingie ndani ya nyumba.

KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP

*********

JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:

KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA

INSTAGRAM: @Globalpublishers

ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo

TWITTER: @GlobalHabari

FACEBOOK: @GlobalPublishers

SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers

GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com

HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz

Leave A Reply