The House of Favourite Newspapers

Joe Biden Aondolewa Uvimbe Kwenye Ngozi Wenye Saratani, White House Yafunguka

0
Rais wa Marekani Joe Biden

Rais wa Marekani Joe Biden ameondolewa uvimbe wa kwenye ngozi wenye saratani mwezi uliopita wakati wa uchunguzi wa kawaida wa afya yake, Ikulu ya White House imesema.

Tishu zote za saratani ziliondolewa na hakuna matibabu zaidi yanayohitajika, daktari wa Biden alisema.

Bwana Biden ataendelea na uchunguzi wa ngozi kama sehemu ya huduma yake ya afya inayoendelea, daktari aliongeza.

Rais huyo, 80, alifanyiwa uchunguzi wa mwili mwezi Februari ambapo Ikulu ya Marekani ilisema ilimpata akiwa mzima na “anafaa kwa ajili ya kazi”.

Kevin O’Connor, daktari wa Biden, aliandika barua iliyotolewa kwa vyombo vya habari siku ya Ijumaa kwamba uvimbe huo uliondolewa kwenye kifua cha Bw Biden mnamo 16 Februari katika Kituo cha Kitaifa cha Matibabu cha Kijeshi cha Walter Reed nje ya Washington DC.

“Hakuna matibabu zaidi yanayohitajika,” alisema, akiongeza kuwa eneo hilo “limepona vizuri” tangu kufanyiwa matibabu.

Ujumbe huo ulisema kwamba aina ya saratani iliyopatikana – ‘basal cell carcinoma’ – kwa kawaida haisambai.

Mnamo Januari, mke wa Biden, Bibi wa Rais Jill Biden, aliondolewa uvimbe mitatu, na miwili kati yao baadaye ilipatikana na seli za saratani ya ‘basal’.

Madaktari wanashauri kwamba njia bora ya kuzuia saratani ya ngozi ni kufunika na kupaka mafuta ya jua, hata wakati wa baridi.

Bidens kwa muda mrefu amekuwa mtetezi hodari wa kupigana na kupona saratani.

Mwana wao kijana mkubwa, Beau, alifariki mnamo 2015 kutokana na saratani ya ubongo.

Bw Biden anatarajiwa kutangaza kuwa atawania muhula wa pili madarakani.

LEMA ATANGAZA VITA na NABII GEORDAVIE -“ANAVUNJA NDOA za WATU na KUSEMA ni MAHABA,NITAPAMBANA NAYE”

Leave A Reply