Jokate, Kiba Hakuna Cha Singo Wala Nini
Stori: Hamida Hassan
ALI KIBA na Jokate wanaonekana kuachana huku wakiwa wameacha deni kwa mashabiki wao kwani baadhi walioongea na safu hii walieleza kuwa, imekuwaje wameshindwa kufanya kolabo wala kuandaa shoo ya pamoja?
“Wale walikuwa wapenzi, wote wanajua muziki, wameshindwa nini kufanya angalau hata kolabo moja?
Achilia mbali hilo, wangeandaa shoo ya kwamba Kiba na Jokate wanapafomu jukwaani mbona ingenoga.
Hawajui kutumia fursa hawa,” alisema Jimmy Carlos wa Kinondoni ambaye ni mdau wa burudani huku akitolea mfano wa namna Zari na Diamond walivyoandaa ile All White Party.