Kagera Yatoa Baraka Kwa Mbaraka Kukipiga Azam FC
KLABU ya Azam FC leo imekubaliana na Klabu ya Kagera Sugar ambapo imeruhusiwa kumchukua mchezaji Mbaraka Yusuph kuichezea timu hiyo ya jijini Dar es Salaam.
Katika taarifa iliyotolewa leo na Ofisa Habari wa Azam, Jaffar Idd, meeleza kuwa timu hiyo ilimsajili mchezaji huiyo kutoka Kagera Sugar kwa kufuata taratibu zote za usajili, huku akidokeza kuwa tayari Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeidhinisha usajili wake kupitia mfumo mpya wa usajili wa kimtandao wa TMS.
Baada ya kikao cha jana makao makuu ya Azam kilichofanyika jana, Kagera Sugar walitoa rukhsa kwa aliyekuwa mchezaji wao huyo kuchezea Azam.
STORI: MUSA MATEJA/GPL