Wiki chache baada ya tukio la mauaji ya watu wanne katika mgodi wa wachimbaji wadogo uliopo eneo la namba 4, Kijiji cha Wisolele Kata ya Segese Tarafa ya Msalala katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga kwenye Plant ya kuchenjua Dhahabu ya Dakires, Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwanasa watuhumiwa 13 na vielelezo mbalimbali.