The House of Favourite Newspapers

Richmond Achukua Fomu Kuwania Urais

0

Mwanasheria Akaro-Simba Richmond amechukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania, kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

 

Simba amekabidhiwa fomu hiyo leo Ijumaa tarehe 10 Julai 2020 katika Makao Makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Uchaguzi Chadema Reginald Munisi.

 

Mtia nia huyo anakuwa wa saba ndani ya Chadema kugombea Urais wa Tanzania, tangu zoezi hilo lianze tarehe 4 Julai 2020. Zoezi hilo litafungwa tarehe 19 Julai mwaka huu.

Leave A Reply