The House of Favourite Newspapers

Kamishna wa Ardhi Apiga ‘Stop’ Umilikishwaji Viwanja Kigamboni

0
Kamishina wa Aridhi Kanda ya  Dar es Salaam Bw. Idrisa Kayera (kushoto) akiongozwa na mmoja wa wakazi wa Kibada anayeishi maeneo hayo.
Kamishina wa Aridhi Kanda ya  Dar es Salaam Bw. Idrisa Kayera na baadhi ya wafanyakazi kutoka Wizara Ya Ardhi, Nyumba Na Maendeleo ya Makazi kanda Dar es Salaam wakijionea mazingira ya eneo hilo.
Kamishina wa Aridhi Kanda ya  Dar es Salaam Bw. Idrisa Kayera (katikati mwenye shati jeupe) na baadhi ya wafanyakazi kutoka Wizara Ya Ardhi, Nyumba Na Maendeleo ya Makazi kanda Dar es Salaam wakijionea mazingira ya eneo hilo.
Wakiondoka eneo hilo

Kamishina wa Aridhi Kanda ya  Dar es Salaam Bw. Idrisa Kayera amesimamisha zoezi la  umilikishwaji wa viwanja vya makazi vilivyopo katika bonde la moringa kitalu 12  Kata ya Kibada Wilaya ya Kigamboni.

Kayera amesimamisha zoezi hilo baada ya kutembelea viwaja hivyo vilivyopo mtaa wa  Moringa Wilaya ya Kigamboni na kugundua kuwa eneo hilo lina asili ya bonde na linalengwa na mikondo ya maji inayotoka maeneo mbalimbali ya mitaa hiyo.

Awali Viwanja hivyo vilitakiwa kupimwa na kumilikishwa kwa wakazi wa wilaya  hiyo, lakini sasa eneo hilo litabadilishwa matumizi na litatumika kwa kilimo cha mjini yaani (Auburn farming)

Kayera amewaomba wakazi wa maeneo hayo kuwa wavumilivu wakati ambao Serikali inaandaa utaratibu mpya wa leseni ili kuwa kodishia wananchi watakaohitaji kufanya shughuli za kilimo Cha mjini katika Viwanja hivyo.

Leave A Reply