KAMPENI: MTULIA AITEKA MAGOMENI KAGERA
Baadhi ya mawaziri waliohudhuria mkutano huo.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wakifuatilia sera zake.
ZIKIWA zimebaki siku chache kuelekea uchaguzi mdogo katika Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, Mgombea Ubunge kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Maulid Mtulia ameiteka Magomeni Kagera baada ya wakazi wa eneo hilo kufurika kwa wingi kusikiliza sera zake ambapo amewambia wakazi hao wampe kura ili aweze kuwatumikia vyema na awaondolea changamoto zilizopo ndani ya jimbo hilo.
Hayo ameyaeleza leo wakati akiwa katika kampeni zake kwenye Viwanja vya Nyasi vilivyopo Magomeni ambapo alikuwa akinadi sera za Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwaomba wananhi wa jimbo hilo kumpa kura.
Amesema kuwa aliacha Ubunge ili ajiunge na chama cha ushindi, chama chenye malengo, chama kinacholeta maendeleo kwa wananchi.
NA DENIS MTIMA/GPL
Comments are closed.