The House of Favourite Newspapers

Kampeni ya Upandaji Miti Yapamba Moto Kijiji cha Green Village Estate Bunju Mabwepande

0
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo (katikati), akielezea namna bora ya upandaji miti  alipoenda   kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu nchini (TFS) , SACC Caroline Malundo, akipanda miti   kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti. Mti hiyo 1000 ilipatikana kwa ufadhili wa TFS Ofisi ya Kinondoni.   Naibu Kamishna alimwakilisha  Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo.
Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi ya Mabwepande Colle Mohamed Senkondo, akipanda mti katika hafla ya kuhitimisha kampeni ya upandaji miti 1000 katika Kijiji cha Green Village Estate, Bunju Mabwepande, Kinondoni, Dar es Salaam hivi karibuni.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo (katikati), akiwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Green Village Estate, Bwana Reeves Ngalemwa (kulia kwake), wakati akiwasili kijijini hapo akimwakilisha Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo,  kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti. Mti hiyo 1000 ilipatikana kwa ufadhili wa TFS Ofisi ya Kinondoni.   Kushoto kabisa ni mwakilishi kutoka Shirika la Watumishi Housing Investment (WHI), Bwana Valentine Arra wamiliki wa kijiji hicho.
Mwenyekiti wa Green Village Estate, Bwana Reeves Ngalemwa akizungumza katika hafla hiyo pamoja na mambo mengine alitoa taarifa ya maendeleo ya kijiji pamoja mkakati endelevu wa  kampeni ya utunzaji wa mazingira kijijini hapo. Alisema tuzo licha ya tuzo iliyozinduliwa kushindanisha wanakijiji ili kumpata mtunza mazingira bora lakini mipango imo mbioni ya kuwa na tuzo yenye wigo mpana wa washiriki wake itakayowashirikisha watu kutoka nje ya kijiji.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo (wa pili kulia), akipokea Tuzo ya Mazingira ya Green Village Estate Mazingira Award 2023 kwa  niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mazingira, Afya na Miundombinu ya kijiji hicho, Dk. Rehema Simba (wa tatu kushoto), wakati akizindua rasmi tuzo hiyo itakayotolewa kila mwaka. Mshindi wa tuzo hiyo atakapatikana kutokana na vigezo vilivyowekwa na kamati hiyo. Lengo ikiwa ni kuhamasisha wanakijiji na wakazi wa maeneo ya jirani umuhimu wa kutunza mazingira kwa njia ya kupanda miti.
Baadhi ya wakazi wa Green Village Estate pamoja na mwakilishi kutoka Watumishi Housing wakipozi mbele ya wapiga picha pamoja na mgeni rasmi na wageni wengine waalikwa mara baada ya kumalizika kwa tukio hilo.

 

Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo, akiwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Green Village Estate, Bwana Reeves Ngalemwa akimwakilisha Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo,wamehitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti. Mti hiyo 1000 ilipatikana kwa ufadhili wa TFS Ofisi ya Kinondoni.

Leave A Reply