The House of Favourite Newspapers

Benki ya Absa Kuendelea Kudhamini Absa Dar City Marathon

0
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), Meneja Mahusiano wa benki hiyo, Theresia Kahesa ( katikati ) pamoja na wakimbiaji wengine wakishiriki mbio za Kilomita 21 za Absa Dar City Marathon

BENKI ya Absa Tanzania imesema itaendelea kudhamini mbio za Absa Dar City Marathon ikiwa kama mdhanini mkuu kutokana na faida za mbio hizo kwa ustawi wa afya za watanzania.

Akizungumza wakati wa mbio hizo zilizotimua vumbi jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa, Obedi Laiser alisema kama Absa wanaamini kukimbia kunaleta fursa nyingi katika maisha ikiwa ni pamoja na afya njema jambo muhimu katika ufanisi wa shughuli za uzalishaji mali.

“Katika kukimbia tunajenga afya zetu, ili tuweze kufanya shughuli zetu, tuweze kuishi kwa muda mrefu, ni dhana mojawapo ambayo sisi Absa tunaiishi na ndio maana tukaungana na The Runners Club ili tuweze kuboresha maisha ya watanzania,” alisema Bwana Laiser.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (kushoto) pamoja na washiriki wengine wakiwa kwenye mazoezi 

Alisema Absa kama benki kongwe kuliko zote Tanzania ikitoa shughuli za kibenki tokea mwaka 1925 ni imani yao kwa kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo, Klabu ya The Runners mbio hizo zitaendelea kukua na kufikia viwango vya Kimataifa.

“The Runners Club ni wabobezi katika marathon na sisi kama Absa ni wabobezi hasa inapokuja katika utoaji wa huduma bora za kibenki hivyo tunaamini kwa pamoja tunaweza kuifikisha marathon hii mbali zaidi,” alisema mkurugenzi huyo.

Katika mbio hizo Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Runners Club, alisema pamoja na mambo mengine mbio hizo zina malengo ya kutangaza vivutio vya utalii wa Jiji la Dar es Salaam na ndio sababu zilianzia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini humo na kuzunguuka katika mitaa na barabara mbalimbali maarufu jijini humo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (katikati) akipozi na baadhi ya washiriki wa mbio hizo muda mfupi baada ya kumalizika mbio hizo.

Zaidi ya wanariadha 3000 kutoka mikoa mbalimbali nchini walipimana ubavu wakishindana katika mbio za km 21, 10 na 5 huku washindi walikabidhiwa zawadi ya za medali na pesa taslimu.

Mshindi wa nne wa Mbio za Absa Dar City Marathon, Oscar Shananga ( kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga mara baada ya kufanyika Kwa kinyang’anyiro hicho jijini Dar es Salaam Jana. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Obedi Laiser. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa mbio hizo ikitoa kiasi cha shs milioni 45 kufanikisha mashindano hayo.
Mshindi wa Kwanza wa Mbio za Absa Dar City Marathon, , Augustino Sulle ( kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser mara baada ya kufanyika Kwa kinyang’anyiro hicho jijini Dar es Salaam Jana. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki hiyo, Aron Luhanga. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa mbio hizo ikitoa kiasi cha shs milioni 45 kufanikisha mashindano hayo. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo walioshiriki mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika Kwa udhamini mkuu wa benki hiyo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi 200 wa Absa walishiriki katika mashindano hayo yaliyoshirikisha wakimbiaji zaidi ya 3000

 

Leave A Reply