Kanye West Ausifia Wimbo wa Wizkid Esssence kama Wimbo Bora Kwenye Historia ya Muziki
RAPPER kutoka Marekani Kanye West ametumia ukurasa wake wa Instagram kutoa hisia zake juu ya wimbo wa Wizkid “Essence” akiutaja kama wimbo bora toka historia ya muziki ianze hadi hii leo.
Wimbo huo ulitoka mwaka 2020, katika Album ya msanii huyo kutoka nchini Nigeria ya “Made in Lagos” ukaanza kupata mafanikio zaidi 2021 ukiuza zaidi ya nakala 2M nchini Marekani na pia umekuwa certified 2x Platnum na RIAA.
Siku ya Jumapili Rapper huyo kupitia ukurasa wake wa Instagramu aliandika hivi akionesha kuusifia sana wimbo huo:
“Best song in the history of music to date”
Katika post hiyo pia Kanye West aliusifia wimbo aliofanya akimshirikisha Beyonce ‘Church girl’ kama wimbo bora katika album yake, pia msanii huyo aliusifia wimbo wa Dj Khaled aliomshirikisha Rick Ross ‘God did’ kama wimbo bora wa mwaka.
Imeandikwa na: Oswald Mwesiga kwa msaada wa Mitandao.