KUFUATIA Jengo la Ofisi yake kuteketea kwa moto juzi Jumapili jioni, Mbunge wa Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete, leo Jumanne, Juni 19, 2018 amefika katika eneo hilo na kujionea hali halisi ilivyokuwa baadaya ajali hiyo mbaya kutokea.
Ridhiwani ameeleza masikitiko yake kutokana na kuunguliwa ofisi zake hizo huku akisema jambo hilo ni mipango ya Mungu hivyo ni lazima kukubariana na hali halisi.
Mbunge huyo amesema; “Nimefika kwenye eneo la Ofisi ya Mbunge iliyoungua. Nimeona jengo lilivyoharibika. Mungu ameumba mitihani na tujifunze kuikabiri.#ChalinzeNiKaziTu.”
“Mtuhumiwa anadaiwa alikuwa akichoma majani jirani na ofisi hiyo ya mbunge na ukashika moto baada ya kumzidi,mtuhumiwa anashikiliwa kwa mahojiano zaidi. Thamani ya mali zilizoungua haijafahamika ambapo jengo hilo limeteketea kabisa kwa moto huo,” amesema Shana.
Comments are closed.