KENDRICK LAMAR APATA MTOTO WA KWANZA
RAPA kutoka pande za Marekani, Kendrick Lamar, amefanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza mwezi huu baada ya kuficha siri katika kipindi chote cha ujauzito wa mchumba wake, Whitne Alford.
Msanii huyo alimkaribisha duniani mtoto huyo wa kike aliyempata na mchumba’ake Whitney. Wawili hao walikutana miaka 10 iliyopita ambapo walificha mahusiano hayo hadi walipoamua kuyaweka kuweka wazi Aprili 2015.
“Sikuweza hata kumwita ni mke wangu. Nilimuona kama rafiki mwema zaidi kwangu. Kifupim ni mtu ambaye nina uwezo wa kumwelezea hofu zangu na akanielewa,” alisema Kendrick.
Miezi saba baadaye, mshindi huyo wa tuzo ya Grammy alithibitisha kuwa yeye na Whitney waliingia kwenye uchumba.
Comments are closed.