Kesi ya Halima Mdee, Kubenea yapigwa Kalenda
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee (katikati) akitoka katika chumba cha kusikiliza shauri lake leo.
Saed Kubenea (katikati) akitoka nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo,Aprili 18, 2016.
Baadhi ya wafuasi wa Chadema wakiongozana na viongozi hao.
KESI ya wabunge wawili kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Halima Mdee wa Jimbo la Kawe na Saed Kubenea wa Jimbo la Ubungo, iliyopangwa kusikilizwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar, imeahirishwa mpaka Mei 2, mwaka huu.
Wabunge hao wanakabiliwa na kesi ya kumjeruhi Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam,Theresia Mmbando kipindi cha Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar.
Na Denis Mtima/GPL