MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemkuta muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ ana kesi ya kujibu katika tuhuma zinazomkabili za kumuua aliyekuwa staa wa Bongo Movie, Steven Kanumba bila kukusudia.
Mapema leo, Mahakamani hapo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Binadamu wa Hospitali ya Muhimbili, alitoa ushahidi wake akiilezea mahakama namna alivyopokea order ya Jeshi la Polisi kumtaka aufanyie uchunguzi mwili wa Kanumba ambapo baada ya kupasua ubongo walikuta mishipa midogo ya damu ikiwa imevujilia kwenye ubongo huku kisogoni kukiwa kumeganda damu.
Baadaye leo ataanza kujitetea mahakamani hapo.
NA RICHARD BUKOS | GPL
Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers
Android ===>Google Play
iOS ===>Apple Store
==