The House of Favourite Newspapers

Kikwete Aongoza Mazishi ya Jaji Msuya Dar

0
Mwili wa aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Upendo Msuya ukishushwa kwenye gari maalum katika makaburi ya Kinondoni Dar kwa ajili ya pumziko la milele.

 

 

RAIS Mstafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete amewaongoza waombolezaji waliofika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam katika kupumzisha mwili wa aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Jaji Upendo Msuya aliyefariki dunia hivi karibuni.

 

Kutoka kushoto ni Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Khamis, Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakiwa makaburini.

Mamia ya waombolezaji walijitokeza kwenye mazishi hayo wakati wa kuupumzisha mwili wa Msuya kwenye nyumba yake ya milele ambapo viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Paramagamba Kabudi na Spika Mstaafu Anne Makinda walijumuika kumsindikiza.

 

…ibada fupi ikiendeshwa kabla ya kupuzisha mwili wa Upendo katika nyumba yake ya milele.

JajiĀ Msuya alifariki Jumatano, Julai 19 akiwa katika Hospitali ya Kairuki alipokuwa amelazwa baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa kiharusi.

 

 

Majaji wakiwa mbele ya jeneza kabla ya mwili wa marehemu kuingizwa kaburini.

Misa ya kumuaga marehemu ilifanyika katika Kanisa la KKKT Wazo leo Jumamosi asubuhi kabla ya kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni.

Marehemu ameacha watoto wanne.

..Kikwete na mama Salma wakiweka udongo kaburini wakati wa mazishi.

 

Mama Salma Kikwete akiweka udongo kaburini.

 

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Paramagamba Kabudi akiweka udongo kaburini.

 

…Prof. Ibrahim Khamis akiweka udongo kaburi la Msuya.

 

Mtoto wa kwanza wa marehemu Upendo Msuya naye akiweka udongo kaburini.

 

Mume wa marehemu, Hilaly Msuya naye akiweka udongo kaburini.

 

NA DEINIS MTIMA | GLOBAL PUBLISHERS

Leave A Reply