The House of Favourite Newspapers

Kiongozi wa kijeshi wa Chad ashinda uchaguzi wa urais

0
Mtawala wa kijeshi wa Chad Mahamat Déby

Mtawala wa kijeshi wa Chad Mahamat Déby ametangazwa mshindi rasmi wa uchaguzi wa urais, na hivyo kuhalalisha kushikilia kwake madaraka.

Jenerali Déby alishinda 61.3% ya kura, kwa mujibu wa baraza la uchaguzi la taifahilo, likitoa matokeo ya muda, huku mpinzani wake wa karibu, Waziri Mkuu Succes Masra, akipata18.53%.

Masra alikuwa ametangaza mapema kwamba amepata ushindi mkubwakatika duru ya kwanza ya upigaji kura, na kwamba ushindi uliibiwa “kutoka kwa watu”.

Jenerali Déby, 40, alitawazwa kama kiongozi wa Chad na jeshi baada ya baba yake, Idriss Déby Itno, kuuawa wakati wa vita na vikosi vya waasi mnamo Aprili 2021.

Ushindi wake unamaanisha kwamba utawala wa miaka 34 wa familia ya Déby utaendelea.

Matokeo ya uchaguzi wa Jumatatu yalitangazwa wiki mbili mapema kuliko ilivyotarajiwa.

Kabla tu ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa, Waziri Mkuu Masra alidai kushinda katika matangazo ya moja kwa moja kwenye Facebook, na kutoa wito kwa wafuasi wake na vikosi vya usalama kupinga kile alichosema ni jaribio la Jenerali Déby “kuiba ushindi kutoka kwa watu”.

“Idadi ndogo ya watu binafsi wanaamini wanaweza kuwafanya watu kuamini kuwa uchaguzi ulishindwa kwa mfumo ule ule ambao umekuwa ukitawala Chad kwa miongo kadhaa,” alisema.

Chad inakuwa nchi ya kwanza kati ya nchi ambazo jeshi lilinyakua mamlaka katika Afrika Magharibi na Kati katika miaka ya hivi karibuni kufanya uchaguzi na kurejesha utawala wa kiraia.

Lakini wakosoaji wanasema kwa kuchaguliwa kwa Jenerali Déby, machache yamebadilika.

Upigaji kura wa Jumatatu kwa kiasi kikubwaulikuwa wa amani lakini takriban mpiga kura mmoja aliuawa, kulingana na vyombo vya habari vya ndani.

Pia kumekuwa na ripoti za upinzani kuhusu dosari siku ya kupiga kura.

Wanasiasa kumi ambao walikuwa na matumaini ya kugombea walitengwa na baraza la katiba kwa sababu ya “kasoro”, ambayo wengine wanasema ilichochewa kisiasa.

Mpinzani mwingine aliyyetarajiwa kuwania urais, na binamu wa Jenerali Déby, Yaya Dillo, aliuawa na vikosi vya usalama mwezi Februari wakati akidaiwa kuongoza mashambulizi dhidi ya Shirika la Usalama la Taifa katika mji mkuu, N’Djamena.

Leave A Reply