The House of Favourite Newspapers

KMC Yawapa Wajeda Dili la Ujenzi wa Uwanja Wao – Video

0
Meya Benjamini Sitta akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo.

MANISPAA ya Kinondoni leo Jumatatu, Januari 27, 2020, imetiliana saini na Jeshi la Wananchi kikosi cha 361 KJ kilichopo Lugalo jijini Dar es Salaam kuanza rasmi ujenzi wa Uwanja wa mpira wa manispaa hiyo uliopo Mwenge Dar, pamoja na ujenzi wa jengo la Utawala litakalojengwa Makao Makuu ya Manispaa hiyo, Magomeni Dar.

Luteni Kanali, David Michael Luoga (kushoto) na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamini Sitta wakibadilishana mikataba baada ya kutiliana saini za kuanza ujenzi huo.

Akizungumza kwenye mkutano na wanahabari baada ya kutiliana saini Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamini Sitta amesema mara nyingi wamekuwa wakiwatumia wanajeshi hao kwenye shughuli mbalimbali za ujenzi na hakuna siku ambayo waliwahi kuwaangusha hivyo anahamini hata  kwenye mradi huo utakuwa na ubora wa kuridhisha na kukamilika kwa wakati.

Wanahabari kazini.

Naye msimamizi wa ujenzi huo kutoka kikosi cha 361 KJ, Luteni Kanali, David Michael Luoga amesema ujenzi huo utaanza hivi karibuni kukamilika mapema iwezekanavyo na kuiomba manispaa hiyo kuwasilisha vifaa vya ujenzi huo kwa wakati.

HABARI:NEEMA ADRIAN | PICHA: RICHARD BUKOS

Leave A Reply