Kourtney Kardashian achekeshwa jina la mtoto wa Kim
Kourtney Kardashian.
DADA wa kwanza wa mwanamitindo na mtangazaji wa kipindi cha Keeping Up With The Kardashians, Kim Kardashian, Kourtney Kardashian ameibuka na kudai alichekeshwa na jina la Saint West aliopewa mtoto wa pili wa Kim.
Kwa mujibu wa Jarida la NY Daily, Kourtney alisema kuwa aliposikia mdogo wake amejifungua hakutaka kuingilia ama kutoa msaada wa jina gani litafaa lakini alipokuja kusikia kuwa amepewa jina la Saint West alicheka sana.
“Angalia majina niliowapa watoto wangu (Mason na Penelope), Hakuna hata moja linalochekesha,” Kourtney aliliambia jarida hilo.
(Imeandaliwa na Andrew Carlos/gpl)