Leseni ya Gazeti la Raia Mwema Yasitishwa
GAZETI la Rai Mwema limesitishiwa leseni ya uchapishaji na usambazaji kwa muda wa siku 30 kuanzia kesho Septemba 6, 2021
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Idara ya huduma za Habari Gerson Msigwa, uamuzi unatokana mwenendo na mtindo wa uandishiwa Habari na Makala ambao kwa kiasi kikubwa unakiuka misingi ya maadili ya taaluma ya Habari kwa kufanya upotoshaji wa mara kwa mara na uchochezi.