Linex ‘ndoa’ yake yasengenywa
Juzikati zilivuja picha zikimuonesha Mwanamuziki Linex akiwa kama vile amefunga ndoa na bonge la msichana.Picha hizo ziliwafanya watu kuhisi aidha jamaa ana ngoma anaifanyia kichupa au amefunga ndoa kwa siri.
Cha kushangaza alipopigiwa simu na paparazi wetu, mara aseme ni kweli ameoa, mara aseme hayo ni mambo yake binafsi ambayo hapendi kuyaanika.
Majibu yake hayo yamewafanya mashabiki wake wamsengenye wakisema kuwa, kama ni kideo si aseme tu na kama ni kweli kavuta jiko kwani kuna ubaya gani wadau wakijua ili wampongeze?
Hata hivyo, wengi wanahisi ni video ya wimbo wake. Acha Tuone!