Live: Mwili wa Dkt. Ng’wandu Waagwa Lugalo
MWILI wa aliyewahi kuwa Mbunge wa zamani wa Jimbo la Maswa na Waziri, Dkt Pius Yasebasi Ng’wandu, umeagwa leo Desemba 23, 2020, katika Hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salam.
Ng’wandu alifariki usiku wa kuamkia Desemba 19, katika Hospitali ya Somanda mjini Bariadi baada ya kupata matatizo ya presha.
Marehemu aliwahi kuwa balozi nchini Japan mwaka 1990 hadi 1993; Waziri wa Sayansi na Teknologia (2000-2008); Mbunge wa Maswa; Waziri wa Ardhi, Maji, Nyumba na Maendeleo ya Miji (1985-1987), na Waziri wa Maji (1987-1990) nafasi ambayo aliishika tena (1996-1999).