Rais Samia Ashiriki Utiaji Saini Mkataba Wa Ujenzi Wa Reli Ya Kisasa (Picha +Video)
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameshuhudia Utiaji Saini Mkataba wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Makutupora (Singida) hadi Tabora km 368 katika kipande cha tatu cha Ujenzi huo mkubwa wa Reli kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza km 1596 leo tarehe 28 Desemba, 2021, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza mbele ya Rais Samia, Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa amesema mkataba huo unahusisha ujenzi wa reli ya SGR kipande cha kuanzia Makutopora hadi Tabora chenye urefu wa kilomita 368 kwa gharama ya dola bilioni 1.98 ambazo ni sawa na shilingi trilioni 4.4 na ujenzi huo utachukua miezi 46.