The House of Favourite Newspapers

LULU Afunguka Sababu za ‘Kupukutika’

0
Elizabeth Michael ‘Lulu’.

 

MSANII kutoka Bongo Muvi, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwa mara ya kwanza amefungukia sababu zinazomfanya kupungua sana mwili kuwa ni kushinda kwa kula matunda pamoja na mazoezi makali ya viungo.

 

Akizungumza na Star Mix, Lulu alisema kuwa, ameamua kupunguza mwili kwa makusudi na kwamba kila siku anashinda akila matunda na kufanya mazoezi magumu ya viungo.

 

“Watashangaa sana kuniona napungua lakini nafanya hivi wala sijashauriwa na mtu ni kuweka tu mwili wangu sawa. Nafanya sana mazoezi, naenda gym kila siku na kuhakikisha muda mwingi nashinda kwa kula matunda kuliko chakula,” alisema Lulu.

Wiki mbili zilizopita, Lulu alizua gumzo katika Ukumbi wa King Solomon, Namanga jijini Dar baada ya kuonekana akiwa amepungua tofauti na zamani.

 

Na Imelda Mtema | IJUMAA | DAR ES SALAAM

Leave A Reply