Lulu Diva Ajimwayamwaya Studio za Global TV Online
MSANII wa Bongo Fleva, Lulu Diva, kwa mara ya kwanza, Alhamisi ya Novemba 24, alipata fursa ya kualikwa katika mahojiano mbalimbali na mwandishi wa Global TV Online, hivyo akatumia muda huo kupiga picha mbalimbali za kumbukumbu na waandishi hao baada na kabla ya mahojiano yao kuanza.
Katika mahiojiano yake na Global TV online, Lulu Diva aliweza kuelezea mambo mbalimbali yahusianayo na maisha yake halisi tangu ajikite kwenye sana ya muziki pamoja na mipango yake mipya kwenye gemu ya muziki huo,huku akielezea faida na hasara alizozipa hata sasa ndani ya gemu hiyo.
Ofisi za Global TV online zipo Sinza Mori ndani ya jengo la Global Group mkabala na Wanyama Hoteli.