The House of Favourite Newspapers

Madrid Yaichapa Juventus 3-0, Huyu Ronaldo ni Balaa!

Klabu ya Real Madrid ya Hispania imeichapa Juventus ya Italia bao 3-0 katika Michuano ya Ligi ya Klabu Bingwa barani Ulaya usiku wa kuamkia leo.

 

Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa nyumbani wa Juventus, Allianz Stadium, mabao ya Madrid yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 3 na 64 huku Marcelo akifunga ukurasa wa mabao kunako dakika ya 72.

Mchezo huo wa raundi ya kwanza unaitengenezea mazingira mazuri Real Madrid kusonga mbele hatua ya nusu fainali endapo italinda matokeo yake katika mzunguko wa pili.

Mbali na Madrid, Klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani imepata ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Sevilla ya Hispania.

 

Sevilla wakiwa katika Uwanja wao wa nyumbani, Estadio R. Sanchez Pizjuan walifungwa magoli hayo na Thiago Alcantara dakika ya 68 na Jesus Navas aliyejifunga 37.

Bao la Sevilla lilifungwa na Pablo Sarabia dakika 31 ya mchezo huo.

 

JUVENTUS (4-2-3-1): Buffon 6; De Sciglio 5, Barzagli 5, Chiellini 6, Asamoah 5 (Mandzukic 69, 5); Khedira 6 (Cuadrado 75, 6), Bentancur 6.5; Costa 5 (Matuidi 69, 6), Dybala 4, Sandro 5; Higuain 6.

BOOKINGS: Bentancur, Dybala

 

OFF: Dybala 67

SUBS: Szczesny, Cuadrado, Marchisio, Rugani, Lichtsteiner.

MANAGER: Max Allegri

REALĀ MADRID (4-3-1-2): Navas 6.5; Carvajal 6.5, Ramos 7, Varane 6, Marcelo 7; Modric 7 (Kovacic 82), Casemiro 6.5, Kroos 7; Isco 8 (Asensio 75, 6); Benzema 6 (Vazquez 59, 6.5), Ronaldo 9.

 

GOALS: Ronaldo 3, 64, Marcelo 72.

BOOKINGS: Ramos, Kovacic.

SUBS: Casilla, Vallejo, Bale, Hernandez.

MANAGER: Zinedine Zidane

REF: Cuneyt Cakir (TUR).

Comments are closed.