The House of Favourite Newspapers

Maeneo Ambayo Mwanamke Yeyote Duniani Haruhusiwi Kukanyaga

0

MATEMBEZI ni jambo zuri sana, linalomuwezesha mtu kuyafahamu maeneo ambayo vinginevyo usingeyajua, hususani wakati wa likizo. Sio tu kwamba kutembea kunatuimarisha bali pia hutupatia ufahamu wa mambo yanayoendelea katika dunia hii, kazi, tamaduni na hata lugha za watu wanaoishi mahali tunapotembelea.

 

Licha ya msisimko wa furaha tunaoupata tunaposafiri , kuna maeneo manane duniani ambako wanawake hawawezi kwenda kutokana na tamaduni na kazi za watu katika maeneo hayo ambazo haziruhusu mwanamke kufika kwenye maeneo hayo.

Vituo vinane vya nyayo za wanawake duniani:

Hekalu la Ayyappan, Sabarimala, India:

Hekalu la Ayyappan linapatikana katika Kerala, nchini India.

Hekalu Ayyappan ni eneo takatifu la la Ibada la Wahindu .

Bandari ya Ayyappan pia inafahamika kama Sabrimala, nan i eneo ambalo ni marufuku kabisa kwakwa wanawake kuingia.

 

Wanawake wenye umri wa kati ya miaka 6 hadi 60 hawaruhusiwi kabisa kukanyaga mguu wao katika kituo hicho. Kwa ujumla wanawake wote wanaopata hedhi wanapaswa kusahau kabisa njia inayoelekea katika hekalu la Ayyappan.

Klabu ya Burning Tree, Bethesda:

 

Burning Tree Club ni eneo lililopo katika Bethesda, nchini Marekani. Wanasiasa hutumia muda mwingi pale , kwasababu walitaka kuwa na muda mwingi wa kujadili siasa. Hata hivyo, Majaji wa Mahakama ya juu zaidi na rais wao pia walikuwa na fursa ya kutembelea hoteli hiyo.

 

Unayajua maeneo mazuri duniani ambayo kutalii ni mwiko? Nyumba ni bure na ni nzuri ,lakini hakuna anayetaka kuishi katika paradiso hii, kunani?

 

Hii ndio maana Sandra Day O’Cornor alikuwa mwanamke wa kwanza kukanyaga katika kituo hicho mwaka 1981. Hatua hiyo ilifuatia baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa jaji wa ngazi ya juu zaidi nchini Marekani.

Kituo cha kupigia kura cha Saudi Arabia na, Vatican City ya Papa:

Inafahamika wazi kwamba haki za wanawake nchini Saudi Arabia zina ukomo ikilinganishwa na haki za wanawake wenzao duniani. Serikali iliwakataza kufanya mambo kama kuendesha magari kwenye barabara za mitaa.

 

Sawa na katika Ufalme wa Saudia na Vatican City katika uchaguzi wa Papa, mwanamke haruhusiwi kufika kwenye kituo cha kupigia kura kuchagua.

Haji Ali Dargah, Mumbai:

Kituo hiki ni mojawapo ya misikiti iliyopo Mumbai, ambamo India haimruhusu mwanamke kuingia.

Eneo hili takatifu limetengwa kwa ajili ya ibada kulingana na imani za waamini wa eneo hilo. Awali, wanawake walikuwa wakiruhusiwa kuingia katika eneo takatifu linaloitwa Haji Aki Dargah. Lakini tangu mwaka 2012, wanawake hawaruhusiwi tena kuingia katika eneo hilo.

Mashindano ya baiskeli yanayofahamika Tour De France:

Miongoni mwa maeneo ambayo mwanamke hapaswi kwenda ni katika mashindano ya Tour De France, ambayo kwa kawaida hufanyika nchini Ufaransa. Ni wanaume tu wanaoshiriki katika mcheo huo wa kila mwaka ambapo washiriki huendesha baiskeli kuzunguka maeneo ya nchi ya Ufaransa.

Viwanja vya soka kote nchini Iraq:

Kama unavyofahamu ni wanawake tu ambao mwanzo walianzisha mchezo wa soka, kabla wanawake hawajacheza mchezo huo wa mpira wa miguu. Lakini katika Iran, ambako wakazi wake wengi ni Waislamu, ni marufuku kuwatazama wanawake uwanjani.

 

Kwa kawaida wanawake hukaa majumbani, na ni  wanaume tu wanaoruhusiwa kuonekana kwenye viwanja vya soka kulingana na sheria ya Iran.

 

Mlima Omine nchini Japan:

Mlima Omine ni eneo kubwa zaidi la kitalii lililopo katika eneo la Nara, nchini Japan. Eneo hili pia ni maarufu sana kwa maeneo yake matatu ambako watu hufanya maombi ya ujasiri ambayo hufanywa na waumini. Lakini mwanamke haruhusiwi kufika kwenye kwenye mlima huo kuabudu, ni wanaume tu wanaofika hapo.

Milima ya Athos Ugiriki

Mlima Athos unaopatikana katika nchi ya Ugiriki pia ni kisiwa muhimu kwa wanaume ambao hawajaoa. Ni wanaume wanaoishi kwenye mlima huu na ambao wamejitolea kuabudu bila kuwajua wanawake wanaoishi katika mlima huu. Hiyo ndio sababu wanawake hawaruhusiwi kufika kwenye eneo hilo la mlima.

 

Leave A Reply