The House of Favourite Newspapers

Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Kesi ya Wabunge 19 Waliofukuzwa Chadema

0

Leo Juni 22, Mahakama Kuu imetupilia mbali kesi ya msingi iliyofunguliwa na wabunge 19 wa viti maalum CHADEMA waliovuliwa uanachama na chama chao la kupinga kuvuliwa uanachama na Baraza Kuu la CHADEMA.

Chadema Iliwafukuza rasmi wabunge hao Mei 12, 2022, kwenye mkutano wao mkuu uliofanyika Mlimani City ambapo baada ya hapo walifungua kesi ya pingamizi katika mahakama kuu ambayo ndiyo imetolewa maamuzi leo.

Wabunge hao 19 wa Chadema waliingia bungeni baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, ambapo Chadema ilijitokeza hadharani mara kadhaa kukanusha kuwa sio wabunge Wao na kwamba hawakuwasilisha majina ya wabunge wao wa viti maalum.

 

Leave A Reply