The House of Favourite Newspapers

Makamu Wa Rais Ashiriki Kumbukizi Ya Hayati Abeid Amani Karume – Picha

0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume katika kumbukizi ya miaka 52 ya kifo chake tarehe 07 Aprili 2024 iliyofanyika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi – Kisiwandui Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameongoza kisomo cha Dua na Hitma ya kumuombea Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, iliyofanyika Afisi Kuu CCM Kisiwandui Zanzibar tarehe 07 Aprili 2024.

Viongozi mbalimbali wameshiriki akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango.

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, viongozi mbalimbali pamoja na familia ya Hayati Sheikh Abeid Amani Karume wakiomba dua mbele ya kaburi la Hayati Sheikh Abeid Amani Karume katika kumbukizi ya miaka 52 ya kifo chake tarehe 07 Aprili 2024 iliyofanyika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi – Kisiwandui Zanzibar.

Makamu Dkt. Philip Mpango akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi pamoja viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini na Chama katika dua ya pamoja ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiondoka katika Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi -Kisiwandui Zanzibar mahali lilipo kaburi la aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume mara baada ya kuhitimishwa dua ya pamoja ya kumuombea Hayati Karume katika kumbukizi ya miaka 52 ya kifo chake tarehe 07 Aprili 2024.

 

Leave A Reply