Makamu wa Rais Mpango Akutana Waziri Jafo
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdori Mpango, akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Selemani Jafo kushoto na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Hamad Hassan Chande kulia, kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais katika makazi yake Jijini Dodoma leo April 2021.
Katika mazungumzo yao Makamu wa RaisĀ Dkt. Mpango, amesisitiza juu ya utekelezaji wa haraka masuala ya changamoto zilizobaki za Muungano na Mazingira ikiwemo suala la mabadiliko ya tabia ya nchi.